Posts

Showing posts from November, 2022

LUGHA 5 ZA MAWASILIANO KATIKA MAHUSIANO (THE FIVE LOVE LANGUAGES)

Image
Katika utafiti uliofanywa na Gary Chapman katika kitabu chake cha       THE FIVE LOVE LANGUAGESii cha mwaka (1995)      Anaeleza kuwa....  Katika maisha ya mahusiano, kila binadamu ana lugha yake ya mawasiliano katika mahusiano.           Unagundua lugha ya mpenzi wako katika mahusiano kupitia kujua ni vitu gani au mambo gani anapenda kufanya kwako, na yeye anafurahia ikiwa utamfanyia.... Zifuatazo ni lugha 5 za mawasiliano katika mahusiano zilizofanyiwa utafiti na (Gary Chapman).... 1️⃣ Lugha ya maneno ya hamasa au uthibitisho.    〰️ Katika mahusiano kuna aina ya mtu anaetumia lugha hii ya mawasiliano katika mahusiano yake.Yeye hutoa maneno ya hamasa na hupenda kupokea maneno ya hamasa pia. Anapenda kusikia maneno ya shukrani, kupongezwa, kujali na kusifiwa ikiwa amefanya jambo fulani katika maisha yake. Aina hii ya mtu asipopata neno la hamasa au uthibitisho kutoka kwako basi ataliomba yeye mwenyewe ili alisik...

Kongamano Kongamano Kongamano

Image
Chuo kikuu Cha Mtakatifu Augostino kilichopo malimbe jijini Mwanza kinawatangazia wanafunzi wake kuwa kutakuwa na kongamano la mafunzo juu ya matumizi ya mitandao ya kijamii kwa wanafunzi wote wa elimu ya juu chuoni hapo siku ya Jumanne tarehe 8/11/2022 kuanzia saa 2:00 asubuhi katika ukumbi wa M15.          Kongamano hilo limebebwa na kauli                 mbiu isemayo "Matumizi Salama ya Mitandao na Maisha Mapya ya Wanafunzi SAUT” Kongamano hilo limeandaliwa na Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) wakishirikiana na uongozi Saint Augustine University of Tanzania(SAUT-Mwanza).  Kongamano hili ni maalum kwa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu hususani mwaka wa kwanza ambao ndiyo wanaanza safari yao ya masomo ya Shahada mbalimbali za Elimu ya Juu.   

BEI YA MAFUTA YAENDELEA KUSHUKA ZAIDI TANZANIA...

Image
TAZAMA BEI MPYA HAPA  Tuesday, November 01, 2022  Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli hapa nchini, bezi hizi zitaanza kutumika kuanzia Jumatano, Novemba 02, 2022 saa 6:01 usiku. EWURA NA RAFAEL MASAU