WABUNGE SASA KUANZA KUFANYIWA 'MASSAGE' BUNGENI KUONDOA UCHOVU WANAPOTUNGA SHERIA

𝙪𝙨𝙞𝙨𝙖𝙝𝙖𝙪 𝙛𝙤𝙡𝙡𝙤𝙬, 𝙣𝙖 𝙩𝙤𝙖 𝙘𝙤𝙢𝙢𝙚𝙣𝙩 𝙮𝙖𝙠𝙤:


Wabunge nchini Kenya wanatazamiwa kuanza kupata huduma za ukandaji 'Massage' katika majengo ya bunge iwapo ripoti iliyowasilishwa na kamati ya Huduma za Vifaa Hitajika Bungeni itapitishwa.

Kamati hiyo ilisema pendekezo hilo ni kwa minajili ya kuimarisha afya ya wabunge kutokana na kukabiliwa na wakati mgumu wanapotunga sheria. 

Kando na hayo, pia inataka kituo cha afya bungeni kikarabatiwe kulingana na sheria za Wizara ya Afya za kuzuia msambao wa corona.

Kamati hiyo inayoongozwa na Mbunge wa Nyaribari Masaba, Ezekiel Machogu ilisema kituo hicho pia kinatakiwa kipanuliwe ili kuongeza vyumba vya ukandaji, kinyozi na ususi. 

"Kitengo cha wanaume kipanuliwe ili kiwe na vyumba vya kutoa ulimwende na mazoezi ya viungo," ilisoma ripoti hiyo.

Kamati hiyo pia inataka kitengo cha wanawake kiwe na huduma za kurembesha kucha na kutengeneza nywele.

 Wafanyakazi wa kituo hicho cha afya watapewa kandarasi ya miaka mitano yenye uwezekano wa kurefusha kulingana na utendakazi iwapo ripot hiyo itapitishwa.

 Chanzo - Tuko News Toka Kenya.

Comments

Popular posts from this blog

PAPA MSOFE AFUTIWA MASHTAKA, AACHIWA HURU

The Ugandan Mixed School Where Boys Wear 'Skirts'