MWANAMKE AUAWA AKITUHUMIWA KUWA MCHAWI SHILABELA USHETU

𝙪𝙨𝙞𝙨𝙖𝙝𝙖𝙪 𝙛𝙤𝙡𝙡𝙤𝙬, 𝙣𝙖 𝙩𝙤𝙖 𝙘𝙤𝙢𝙢𝙚𝙣𝙩 𝙮𝙖𝙠𝙤:


Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga George Kyando

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Mwanamke aliyejulikana kwa jina la Mwalu Charles (45) mkazi wa kijiji cha Shilabela kata ya Ulewe wilayani Kahama mkoani Shinyanga amefariki dunia baada ya kukatwa na kitu chenye makali sehemu za mgongoni, kichwani na mkono wa kulia na watu au mtu wanaotafutwa akituhumiwa kuwa mchawi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP George Kyando amesema tukio hilo limetokea Septemba 9,2021 majira ya saa mbili usiku katika kijiji cha Shilabela, kata ya Ulewe, tarafa ya Mweli ,wilaya ya kipolisi Ushetu, wilaya ya Kahama mkoa wa Shinyanga.

“Mwalu Charles (45) mkazi wa kijiji cha Shilabela, alikufa kwa kukatwa na kitu chenye makali sehemu za mgongoni, kichwani na mkono wa kulia na watu au mtu wanaotafutwa”,amesema.

Amesema kiini cha tukio ni mgogoro wa kifamilia unaochochewa na imani za kishirikina ambapo marehemu alikuwa akituhumiwa kuwa mchawi.

Amesema tayari watuhumiwa watatu wamekamatwa.

Comments

Popular posts from this blog

PAPA MSOFE AFUTIWA MASHTAKA, AACHIWA HURU

The Ugandan Mixed School Where Boys Wear 'Skirts'