Mauaji Mbezi: Afisa Mtendaji Achinjwa Akiwa Ofisini kwake oct 13, 2021

𝐅𝐎𝐋𝐋𝐎𝐖 𝐏𝐀𝐆𝐄 𝐍𝐀 𝐓𝐎𝐀 𝐂𝐎𝐌𝐌𝐄𝐍𝐓 𝐘𝐀𝐊𝐎 𝐇𝐀𝐏𝐎 𝐂𝐇𝐈𝐍𝐈👇👇
 

Mauaji ya kutisha yametokea eneo la Mbezi Msumi mkoani Dar es Salaam baada ya watu wasiofahamika kudaiwa kuvamia ofisi za Serikali ya Mtaa wa eneo hilo na kisha kumuua Ofisa Mtendaji kwa kumkata na panga.

Tukio hilo la mauaji limetokea leo Oktoba 11, 2021 kati ya saa sita hadi saa saba mchana wa leo na inadaiwa ofisa huyo mtendaji wa Serikali ya Mtaa wa Mbezi Msumi Jijini Dar es salam ameshambuliwa kwa kukatwa na panga shingoni na watu ambao hawafahamiki.


Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za mauaji ya mtendaji wa mtaa wa Mbezi Msumi, aliyejulikana kwa jina la Kelvin Costa Mowo (38), wakati akitekeleza majukumu yake ya kusikiliza wananchi ambao walikuwa na mgogoro wa ardhi.

Kelvin aliuawa dunia jana Jumatatu, Oktoba 11, 2021 majira ya saa 5:54 baada ya watu wasiojulikana kumvamia ofisini na kuanza kumshambulia kwa mapanga mpaka kusababisha kifo chake.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema watuhumiwa wengine bado wanasakwa ili kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Comments

Popular posts from this blog

Kauli ya Serikali Kuhusu Bei ya Mafuta

INASIKITISHA!! MAPACHA WAFARIKI MAMA YAO MZAZI AKIWA BIZE FACEBOOK September 22,2021

The ancients said that the way you feed a child is the way he/she grow up.